Tuesday, July 31, 2012

BAADA YA KUTILIWA MASHAKA KUTOKANA NA REKODI ALIYOIWEKA YA KUOGELEA KWA KASI ZAIDI KULIKO KAWAIDA SWIMMER SUPERGIRL (YE SHIWEN) APIMWA KAMA ALITUMIA UDANGANYIFU WOWOTE WA KUTUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU!



Baada ya kuhisi kuwa mchina Ye Shiwen (16) atakua ametumia madawa ya kuongeza nguvu apimwa na kuonekana safi. 

Mwenyekiti wa Chama cha michezo ya Olimpiki ya Uingereza amesema, baada ya shaka la  kocha wa Marekani (John Leonard ) kutolewa kuhusiana na kuwa mtu wa kawaida hawezi kuogelea kwa kasi aliyoonesha Ye Shiwen na kuvunja rekodi ya dunia waliamua kumpima na majibu kuonekana hakuwa na matumizi yoyote ya kutumia dawa za kuongeza nguvu hivyo anastaili kutambulika ulimwenguni kwa rekodi hiyo.
Kocha huyo  wa Marekani alisema kitendo cha kuogelea kwa kasi hiyo kulimchanganya na kuisi kuwa kuna swala hilo la kutumia madawa. Kwani  kitendo cha Ye Shiwen,kilimkumbusha waogeleaji wa Ujerumani Mashariki wanawake katika miaka ya 1980, ambao walitumia  madawa.

Ye Shiwen amevunja rekodi  ya dunia kwa kuogela ndani ya sekunde 28:93 umbali wa m50 na kumpita mmarekani  mwanaume ryan lochte(27) kwa sekunde mbili zaidi ambaye alishikilia rekodi hiyo kwenye mashindano ya olympics

No comments: