![]() |
| Raisi wa sasa wa Ghana, John Dramani Mahama |
![]() |
| Zoezi la kuapishwa. |
![]() |
| Raisi John Atta mills enzi za uhai wake |
John Dramani Mahama usiku wa jana apishwa kuwa Rais wa
Jamhuri ya Ghana na Amiri Jeshi Mkuu wa Vikosi vya Jeshi nchini Ghana,
ambapo anachukua nafasi ya marehemu Rais Evans Atta Mills, ambaye alifariki
dunia katika Hospitali ya Jeshi mchana Jumanne 24, baada ya kuugua kwa muda
mfupi.
Kama ilivyoainishwa katika kifungu cha 60 (6) ya Katiba ya 1992 ya Ghana, Jaji Mkuu Georgina Theodora Wood wa Ghana alisimamia zoezi zima la kiapo cha Makamu huyo wa zamani wa Raisi, ambapo katika zoezi hilo kulitanda hisia za Majonzi.
Mara baada ya kuapishwa Raisi Mahama Alisema: "Kwa mara ya kwanza katika historia ya Ghana, tumepoteza rais aliyepo madarakani ambaye alifanya kazi bila kuchoka kwa ajili ya watu wake".
Rais Mahama alisema kamwe hakufikiri kuwa angeweza kuongoza taifa katika kipindi kigumu kama hiko na kuwasihi wa Ghana kudumusha umoja na utulivu wa Taifa ". Raisi Atta Mills amefariki akiwa na umri wa miaka 68. Mungu ampumzishe kwa Amani.
Kama ilivyoainishwa katika kifungu cha 60 (6) ya Katiba ya 1992 ya Ghana, Jaji Mkuu Georgina Theodora Wood wa Ghana alisimamia zoezi zima la kiapo cha Makamu huyo wa zamani wa Raisi, ambapo katika zoezi hilo kulitanda hisia za Majonzi.
Mara baada ya kuapishwa Raisi Mahama Alisema: "Kwa mara ya kwanza katika historia ya Ghana, tumepoteza rais aliyepo madarakani ambaye alifanya kazi bila kuchoka kwa ajili ya watu wake".
Rais Mahama alisema kamwe hakufikiri kuwa angeweza kuongoza taifa katika kipindi kigumu kama hiko na kuwasihi wa Ghana kudumusha umoja na utulivu wa Taifa ". Raisi Atta Mills amefariki akiwa na umri wa miaka 68. Mungu ampumzishe kwa Amani.



No comments:
Post a Comment